Mkuu wa Shule
Namna ya kuingia kwenye mfumo
Baada ya kusajiliwa na Afisa TEHAMA wa HALMASHAURI, anza kwa kufungua kivinjari chako katika kompyuta ambacho kimeunganishwa katika mtandao wa internet. Kivinjari hicho kinaweza kuwa Google Chrome, Mozila Firefox au Microsoft Edge.
Kisha aandika anuani ifuatayo sis.tamisemi.go.tz. Anza kwa kuingiza “Username” na “Password” uliyotengenezewa na Afisa TEHAMA wa HALMASHAURI. Kisha Bofya kitufe kilicho andikwa “INGIA” ili uweze kuingia kwenye mfumo.
Mara baada ya mfumo kufunguka kwa mara ya kwanza utatokea ukurasa unaokutaka kubadilisha neno la siri. Andika neno la siri (Default Password) ambayo ni secret, kisha andika neno jipya la siri na kulihakakiki. Baada ya hapo Hifadhi taarifa zako. Mfumo utakuotoa nje na kukutaka uingie tena, weka barua pepe na nywila mpya kisha bofya kitufe kilichoandikwa ingia.
Mara baada ya mfumo kufunguka kwa mara ya kwanza huu ndio utakuwa ukurasa wa kwanza unaoonyesha menyu zitakazofanyiwa kazi na Mkuu wa Shule.