Mwalimu wa Darasa

Namna ya kuingia kwenye mfumo

Baada ya kusajiliwa na Mkuu wa Shule, anza kwa kufungua kivinjari chako katika kompyuta  ambacho kimeunganishwa katika mtandao wa internet. Kivinjari hicho kinaweza kuwa Google Chrome, Mozila Firefox au Microsoft Edge.

alt Imange Description

Kisha aandika anuani ifuatayo sis.tamisemi.go.tz. Anza kwa kuingiza “Username” na “Password” uliyotengenezewa na Mkuu wa Shule. Kisha Bofya kitufe kilicho andikwa “INGIA” ili uweze kuingia kwenye mfumo.

alt Imange Description

Mara baada ya mfumo kufunguka kwa mara ya kwanza utatokea ukurasa unaokutaka kubadilisha neno la siri. Andika neno la siri (Default Password) ambayo ni secret, kisha andika neno jipya la siri na kulihakakiki. Baada ya hapo Hifadhi taarifa zako. Mfumo utakuotoa nje na kukutaka uingie tena, weka barua pepe na nywila mpya kisha bofya kitufe kilichoandikwa ingia.

alt Imange Description

Mara baada ya mfumo kufunguka kwa mara ya kwanza huu ndio utakuwa ukurasa wa kwanza unaoonyesha menyu zitakazofanyiwa kazi na Mwalimu wa Darasa.

alt Imange Description

Panga Wanafunzi kwenye Mikondo

Baada ya kupewa majukumu ya Mwalimu wa Darasa yaani Class Teacher na kupangiwa darasa na Mkuu wa Shule Mwalimu wa Darasa ataanza kupanga wanafunzi kwenye mikondo aliyopangiwa na Mkuu wa Shule na kisha atabofya kitufe kilichoandikwa HIFADHI kama inavyoonekana hapa;

alt Imange Description

Orodha ya Wanafunzi kwenye mkondo

Mwalimu wa Darasa anaweza kuangalia orodha ya wanafunzi waliopangwa kwenye mkondo kama inavyoonekana;

alt Imange Description

Orodha ya Wanafunzi

Mwalimu wa Darasa pia anaweza kuangalia orodha ya wanafunzi kama inavyoonekana hapa;

alt Imange Description

Chukua Mahudhurio ya Wanafunzi

Mwalimu wa Darasa anajukumu la kuchukua mahudhurio ya wanafunzi katika darasa husika kwa kipindi/ muda wa masomo (Asubuhi/Mchana). Katika mchakato wa kuchukua mahudhurio Mwalimu wa Darasa anao uwezo wa kuweka sababu kwa wanafunzi wote ambao watakuwa hawajafika/ kuhudhurio kipindi hicho. Kutokana na baadhi ya madarasa kuwa na wanafunzi wengi, mfumo unamuwezesha Mwalimu wa Darasa kuweza kuweka alama ya TICK kwenye kichumba kilichowekewa alama ya namba 4 ili kuweza kuonyesha kwamba wanafunzi wote wapo na baada ya hapo kuanza kuondoa alama hiyo kwa wale ambao hawapo sambamba na kuweka sababu kama inavyoonekana hapa;

alt Imange Description

Baada ya kuchukua mahudhurio Mwalimu wa Darasa atatakiwa ahifadhi mahudhurio hayo kama inayoonekana hapa;

alt Imange Description

Hariri Mahudhurio

Mfumo unamuwezesha MWalimu wa Darasa kuweza kuhariri Mahudhurio kama inavyoonekana hapa;

alt Imange Description

Pangia Wanafunzi Masomo

Mfumo unamuwezesha Mwalimu wa Darasa kuwapangia wanafunzi masomo kama inavyoonekana hapa;

alt Imange Description

Wanafunzi Waliopangiwa Masomo

Mfumo unamuwezesha Mwalimu wa Darasa kuangalia wanafunzi waliopangiwa masomo kama inavyoonekana hapa;

alt Imange Description

Mwisho wa Moduli ya Mahudhurio